Mtaa wa Kinondoni Dunga
Dar es Salaam
Sisi ni jumuiya
ya Imani na Upendo
Tupo kuwaongoza watu katika uhusiano unaokua na Yesu Kristo. Sisi ni kanisa linaloamini Biblia, lililojitoa kwa ibada ya moyo, uanafunzi, na kulitumikia jiji letu la Dar es Salaam.
Iwe unachunguza imani au unatafuta kanisa la nyumbani, utapata jumuiya ya ukaribisho kwa familia, vijana, na watu wa kila hali ya maisha.
Jiunge Nasi
Tukilitumikia jamii ya Kinondoni
Jiunge Nasi Wiki Hii
Ibada za Jumapili
Saa 1:00 Asubuhi na Saa 4:30 Asubuhi
Ibada ya CMF na WWK
Jumatatu Saa 10:30 Jioni
Mkesha wa Maombi
Jumanne Saa 1:00 Usiku - Saa 4:00 Usiku
Ibada ya Katikati ya Wiki
Jumatano Saa 10:30 Jioni
Ibada ya Vijana ya CAs
Alhamisi Saa 11:00 Jioni
Mkesha Wa Ijumaa
Duru ya Kwanza 07:00 Usiku - 4:00 Usiku, Duru ya Pili 4:00 Usiku - 10:00 Asubuhi
Nini cha Kutegemea
Unakuja kwa mara ya kwanza? Haya ndiyo unayohitaji kujua kuhusu ibada zetu.
Nivae nini?
Njoo ulivyo. Watu wengi huvaa smart casual, lakini unakaribishwa katika mavazi yoyote unayojisikia vizuri.
Ibada huchukua muda gani?
Ibada zetu kwa kawaida huchukua takriban dakika 90, zikiwa na ibada, maombi, na ujumbe wenye msaada wa maisha.
Idara ya Watoto?
Tuna mazingira salama, ya kufurahisha, na yenye kuwajenga watoto wako kumjua Mungu wakati wewe unahudhuria ibada.
Tufatilie Mtandaoni
Huwezi kuungana nasi ana kwa ana? Pata ibada zetu mtandaoni.
IBADA YA JUMATANO | 4 MACHI 2026 | 2026 | KINONDONI REVIVAL CHURCH
person Kinondoni Revival Church
calendar_today May 23, 2026
"IBADA YA JUMATANO | 4 MACHI 2026 | 2026 | KINONDONI REVIVAL CHURCH"
Angalia Sasa arrow_forwardKaribu Nyumbani
Askofu Dkt. Rogathe Swai | Mchungaji Kiongozi
"Kwa niaba ya kusanyiko takatifu la wakristo wa Kanisa la Uamsho la Kinondoni, Mimi Mchungaji Kiongozi Askofu Dkt. Rogathe Z. Swai kwa furaha na uhakika napenda kumthibitishia kila Mtanzania, wageni na watu wote katika sayari hii ya dunia yetu kwamba, kwa neema ya Mungu kanisa letu limefanyika kuwa ‘’Mahakama ya Rufaa na “Hospitali ya Rufaa’’ kwa watu wenye shida, mateso, vifungo vya nguvu za giza. Zaidi, Mungu amelifanya Kanisa kuwa ‘’Nyumba ya Nuru’’ kutoa ufahamu na hekima ya Ki Mungu kwa Watakatifu wengi na pia faraja kwa Wahitaji kimaisha. Kwa sababu hizi na nyingine nyingi, mimi Mchungaji Kiongozi kwa niaba ya kanisa, tunawakaribisha wote kujumuika nasi katika ibada zetu za sifa, mahubiri, maombi na maombezi na mafundisho yaliyojaa kweli kuu za injili ya Kristo Yesu pamoja na upako mwingi wa nguvu zitendazo kazi za Roho Mtakatifu wa Mungu aishiye katika maisha ya watu wake."
Zaidi, Mungu amelifanya Kanisa kuwa ‘’Nyumba ya Nuru’’ kutoa ufahamu na hekima ya Ki Mungu kwa Watakatifu wengi na pia faraja kwa Wahitaji kimaisha. Kwa sababu hizi na nyingine nyingi, mimi Mchungaji Kiongozi kwa niaba ya kanisa, tunawakaribisha wote kujumuika nasi katika ibada zetu za sifa, mahubiri, maombi na maombezi na mafundisho yaliyojaa kweli kuu za injili ya Kristo Yesu pamoja na upako mwingi wa nguvu zitendazo kazi za Roho Mtakatifu wa Mungu aishiye katika maisha ya watu wake."
"Maono yetu na mwelekeo(our focus) wetu ni kumhubiri Kristo Yesu kwa Taifa la Tanzania na kwa watu wa kizazi chetu ili kumvunia Mungu wetu mavuno mengi, kisha kuwafundisha waaminio juu ya maisha ya Ibada ya kweli na utumishi wa bidii na uaminifu kwa Bwana wakati huohuo kanisa likeshe, kuwa macho kumngoja Bwana Yesu kwa maana ya kusubiri kurudi kwa mara ya pili. Jiunge nasi katika safari ya imani."
Idara Zetu
Pata nafasi yako ya kuhudumu na kukua
CMF
Maono ya kuwako kwa Ushirika wa Wanaume Wakristo, yaani Christian Men’s Fellowship (CMF) una historia ndefu katika TAG. Kwanza, wazo lilianza kama shauku ya uongozi wa Kanisa kitaifa, Pili, ilitokana na hitaji la wanaume wenyewe, na vilevile lilikuwa ombi la muda mrefu kutoka kwa Idara ya Wanawake Watumishi wa Kristo (W.W.K) wa kanisa letu. Mwaka 2008, wakati wa awamu ya tatu ya uongozi wa kanisa chini ya Askofu Dr. Barnabas Mtokambali, TAG ilitengeneza Dira ya Maendeleo ya Kanisa ya utekelezaji wa miaka kumi ya mavuno. Katika Eneo C linalosema “Inua viwango vya Ibada ya binafsi na pamoja”, kipengele cha C4:5-kina mkakati unaosema, “Anzisha Idara ya Wanaume”.
Jifunze Zaidi arrow_forward
WWK
Idara ya Wanawake imeanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 20 sehemu ya 7 ya katiba ya Tanzania Assemblies of God. Hivyo kutokana na msingi huo Idara ya WWK imeandaa taratibu na muongozo wa Idara ya WWK kwa msingi wa kuongoza na kusimamia shughuli zote za Idara hii.
Jifunze Zaidi arrow_forward
CA's
Jina la Idara ni Tanzania Assemblies of God - Christ's Ambassadors (CA's); Yaani ikiwa na maana ya Vijana mabalozi wa Kristo.'Kimsingi ni Idara ya Vijana'.
Jifunze Zaidi arrow_forward
Watoto
Idara ya Watoto na Wanafunzi ni Idara ndani ya kanisa la TAG, lilianzishwa rasmi Mwaka 1994 kufuatia mkutano wa viongozi wa Kanisa la Assemblies of God, barani Afrika, “Africa Assemblies of God Alliance” (AAGA) uliofanyika Nairobi, nchini Kenya mwaka mwaka 1993. Idara hii ilianzishwa ikiwa ni utekelezaji wa maazimio muhimu katika mkutano huo wa (AAGA). Mwaka huo wa 1994 kanisa la TAG lilikuwa linaongozwa na Askofu Mkuu Rev. Ranwell Mwenisongole na alimteua marehemu Mchungaji Joseph Justine kuwa Mkurugenzi Mkuu. Kadhalika, marehemu Mchungaji Jeremiah Kimaro aliteuliwa kuwa Makamu Mkurugenzi Mkuu na Mch. Everhard Mloka kuwa Katibu Mkuu. Huo ndio ukawa mwanzo mzuri wa Idara hii.
Jifunze Zaidi arrow_forward
Matukio Yajao
Usikose yanayoendelea kanisani kwetu
Hakuna matukio yajayo kwa sasa
"Kanisa hili limesaidia familia yangu kukua kiroho na kupata jumuiya ya kweli ya waumini."
- Mwanachama wa Kanisa
"Watu wakarimu, ibada yenye nguvu, na mafundisho imara ya Biblia yanayobadilisha maisha."
- Mgeni wa Mara ya Kwanza
"Mahali ambapo imani huwa halisi na hai kupitia kulitumikia jamii yetu ya karibu."
- Mjitoleaji
Shirikiana Nasi Katika Utume
Ukarimu wako unawezesha huduma, ufikishaji, na uenezaji wa Injili ndani ya Dar es Salaam na kwingineko. Pamoja, tunaleta athari ya milele.
volunteer_activism Toa Sadaka kwa Usalama
Jiunge Nasi Jumapili Hii
"Tunakualika kwa moyo wote kuabudu pamoja nasi. Pata upendo wa Mungu, ushirika na waumini, na ukue katika imani yako ndani ya jumuiya inayojali."