Matangazo ya Kanisa 01 - 07 June 2026
arrow_back All Announcements
weekly push_pin Pinned

Matangazo ya Kanisa 01 - 07 June 2026

calendar_today May 31, 2026 person Super Admin
picture_as_pdf

Attachment Available

VFVak1uz4Q3HmCyDTYeOKJOJ56kzBstaCjAo80QR.pdf

download Download PDF
VIONGOZI WA ZAMU 
 01 –07 JUNI 2026 

MCHUNGAJI REV. WITNESS SWAI 0629 534 530 

MZEE WA KANISA: 
MR. REMIGIUS NGAIZA 

WAZEE NA MAKATIBU WAO WATAKAOKU WA ZAMU, KUABUDU IBADA ZOTE MBILI SIKU YA JUMAPILI IJAYO TAREHE 07/06/2026: 

MR. RODERICK LUTEMBEKA 
MRS.RHODA BUNDARA 
MCH. GREYSON NYANTAMBA 

MASHEMASI WA ZAMU: 

MR. GREGORY MUSHI 
MR. HOSEA NTUNUNGURU 
MRS IDDA MHINA 
MR. ISACK SAKARANI 

MATANGAZO 

Wazee wote wenye mitaa mnahimziwa kutembelea vituo vyenu vya HBCF ili kujua maendeleo ya vituo hivyo na kuviimarisha, wakisaidiana na makatibu pamoja na mashemasi. 

Kutakuwa na Ibada ya shukrani ya nusu mwaka pamoja na Ushirika wa meza ya Bwana tarehe 28.06.2026. Washirika wote tujiandae na ibada hiyo yenye baraka. 

Mchungaji kiongozi anakumbusha tena kuwa vijana ambao wako kwenye mahusiano ya uchumba wasikae zaidi ya miezi mitatu bila kuonana na Mch. Dickson Mkoka pia wajitambulishe kwenye kamati ya kushauri chumba na kuhudhuria kwenye vikao vya chumba.

MICHANGO YA FEDHA ZA UJENZI 

1.Kwa neema ya Mungu ujenzi wa kanisa letu unaendelea, hivyo unatiwa moyo wewe uliye ahidi mchango wa ujenzi kwa awamu hii ya sita B kutoa au kupunguza ahadi yako ili kazi ya ujenzi iendele. Kumjengea Mungu nyumba ya ibada ni baraka kwako na kwa vizazi vyako. 

2.Unaweza kutuma mchango wako kwenda namba: 
 015 0020374000 CRDB BANK. Jina: KINONDONI REVIVAL CHURCH 
PAA LA KANISA, MUUJIZA WANGU 

TANGAZO IDARA YA WATOTO 

Tarehe 12.06.2026 : Mkesha wa kusifu na kuabudu, maombi na kuonyesha vipaji vya watoto na maombi ya ujazo wa Roho Mtakatifu. Mzazi njoo tuwaombee watoto wetu. 

Tarehe 15– 21 Juni 2026 wiki ya Idara ya watoto na wanafunzi, kutakuwa na makambi hapa kanisani kuanzia saa 8 mchana hadi saa 12 jioni Ibada ya Jumatano na Ijumaa (HBCF) zitaongozwa na Idara ya watoto.Njoo na familia yako yote upokee kutoka kwa Bwana. 

Tarehe 21.06.2026 ni kilele cha sikukuu ya watoto, sare ziko tayari (Tshirt) bei ni Tzs 10,000. 

TANGAZO LA NDOA 

Kwa mara ya pili tunatangaza harusi kati ya kaka Jovin Jonathan Jovitha na dada Emiliana Bruno Kipeto wote ni washirika wa TAG Kinondoni .Harusi itafanyika siku ya Jumapili tarehe 14/06/2026 hapa kanisani TAG Kinondoni. 

KUWEKA WAKFU WATOTO 

Jumapili ya tarehe 07.06.2026 kutakuwa na ibada ya kuweka wakfu watoto hivyo kwa mshirika yoyote ambaye bado hajaleta mtoto wake, anakaribishwa.